61. Wakamwambia, “Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?”
62. Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.
63. Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: “Yohane ndilo jina lake.” Wote wakastaajabu.
64. Papo hapo, midomo na ulimi wake Zakaria vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.