20. Amramu alimwoa Yokebedi, shangazi yake, naye akamzalia Aroni na Mose. Amramu aliishi miaka 137.
21. Na watoto wa kiume wa Ishari walikuwa: Kora, Nefegi na Zikri.
22. Watoto wa kiume wa Uzieli walikuwa: Mishaeli, Elsafani na Sithri.
23. Aroni alimwoa Elisheba, binti yake Aminadabu, dada yake Nashoni; naye akamzalia Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
24. Nao watoto wa kiume wa Kora walikuwa: Asiri, Elkana na Abiasafu, ambao walikuwa mababu wa jamaa za Kora.