Kutoka 6:20-24 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Amramu alimwoa Yokebedi, shangazi yake, naye akamzalia Aroni na Mose. Amramu aliishi miaka 137.

21. Na watoto wa kiume wa Ishari walikuwa: Kora, Nefegi na Zikri.

22. Watoto wa kiume wa Uzieli walikuwa: Mishaeli, Elsafani na Sithri.

23. Aroni alimwoa Elisheba, binti yake Aminadabu, dada yake Nashoni; naye akamzalia Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.

24. Nao watoto wa kiume wa Kora walikuwa: Asiri, Elkana na Abiasafu, ambao walikuwa mababu wa jamaa za Kora.

Kutoka 6