Kutoka 4:29-31 Biblia Habari Njema (BHN)

29. Kisha Mose na Aroni wakaenda, wakawakusanya wazee wote wa Waisraeli.

30. Aroni akawaambia maneno yote Mwenyezi-Mungu aliyokuwa amemwagiza Mose, na kuifanya ile miujiza mbele ya watu wote.

31. Watu wakaamini. Na waliposikia kwamba Mwenyezi-Mungu amewajia kuwasaidia Waisraeli, na kwamba ameyaona mateso yao, wote wakainamisha vichwa vyao na kumwabudu.

Kutoka 4