Kutoka 29:7-11 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Baada ya kufanya hivyo, utachukua yale mafuta ya kupaka, ummiminie Aroni kichwani mwake kumweka wakfu.

8. “Kisha utawaleta wana wa Aroni na kuwavika vizibao.

9. Utawafunga mishipi viunoni na kuwavisha kofia zao. Hivyo ndivyo utakavyowaweka wakfu Aroni na wanawe kuwa makuhani. Hao watakuwa makuhani daima.

10. “Kisha utamleta yule ndama dume mbele ya hema la mkutano. Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa cha ndama huyo

11. na kumchinja mbele ya Mwenyezi-Mungu, mlangoni pa hema la mkutano.

Kutoka 29