13. Utatengeneza mipiko ya mjohoro na kuipaka dhahabu.
14. Mipiko hiyo utaipitisha katika pete zilizo pande mbili za sanduku, kwa ajili ya kulibebea.
15. Mipiko hiyo itabaki daima katika pete; isitolewe wakati wowote.
16. Ndani ya sanduku hilo utaweka vibao viwili vya mawe vya ushuhuda.
17. “Kisha utatengeneza kwa dhahabu safi kiti cha rehema, urefu wake sentimita 110, na upana wake sentimita 66.
18. Utatengeneza pia mfano wa viumbe hai viwili kwa kufua dhahabu, uviweke kwenye miisho miwili ya kiti hicho;
19. kiumbe kimoja mwisho mmoja na kiumbe kingine mwisho mwingine. Viweke viumbe hivyo kwenye miisho ya kiti hicho, lakini viwe kitu kimoja na hicho kiti.