17. Baba wa huyo msichana akikataa katakata kumwoza binti yake, mtu huyo atalipa fedha ya mahari inayostahili msichana aliye bikira.
18. “Usimwache mwanamke mchawi aishi.
19. “Anayezini na mnyama lazima auawe.
20. “Anayemtolea tambiko mungu mwingine badala ya Mwenyezi-Mungu pekee, lazima aangamizwe kabisa.
21. “Msimdhulumu mgeni wala kumtesa, maana nanyi pia mlikuwa wageni nchini Misri.
22. Msimtese mjane au yatima.
23. Kama mkiwadhulumu hao nao wakanililia, hakika nitakisikiliza kilio chao,