Kutoka 17:14-16 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Kisha Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Liandike jambo hili katika kitabu, liwe ukumbusho. Tena kariri masikioni mwa Yoshua kwamba nitawafuta kabisa Waamaleki duniani.”

15. Mose akajenga madhabahu na kuiita, “Mwenyezi-Mungu ni Bendera Yangu”,

16. akisema, “Inueni juu bendera ya Mwenyezi-Mungu! Mwenyezi-Mungu atapigana na Waamaleki kizazi hata kizazi!”

Kutoka 17