1. Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose na Aroni, walipokuwa bado nchini Misri,
2. “Mwezi huu utakuwa kwenu mwezi wa kwanza wa mwaka.
3. Iambieni jumuiya yote ya Waisraeli kwamba mnamo siku ya kumi ya mwezi huu, mtachukua mwanakondoo mmoja kwa kila jamaa moja.
4. Kama jamaa moja ni ndogo mno hata isiweze kumaliza kondoo mmoja, itashirikiana na jamaa jirani kadiri ya idadi ya watu wake; kisha watachagua mnyama ambaye kila mtu ataweza kula.