9. Kumbukeni Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu alivyomtendea Miriamu mlipokuwa safarini kutoka Misri.
10. “Ukimkopesha jirani kitu chochote, usiingie kwake kuchukua rehani.
11. Msubiri nje na umwache yeye mwenyewe akuletee hiyo rehani.
12. Kama yeye ni maskini usikae na rehani hiyo usiku kucha.