Isaya 8:8-13 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Utaingia nchini Yuda kwa nguvu na kufurika na kupanda mpaka shingoni; utaenea juu ya nchi yako yote, ee Emanueli!”

9. Unganeni enyi watu wa mataifa nanyi mtafedheheshwa!Sikilizeni enyi nchi za mbali duniani!Jiwekeni tayari na kufedheheshwa;naam, kaeni tayari na kufedheheshwa.

10. Shaurianeni pamoja lakini itakuwa bure;fanyeni mipango lakini haitafaulu,maana Mungu yu pamoja nasi.

11. Mwenyezi-Mungu alinionya kwa nguvu nisifuate njia za watu hawa, akaniambia,

12. “Usijumuike nao katika njama zao, wala usiogope yale wanayoyaogopa wala kuwa na hofu.

13. Nitambue mimi peke yangu, Mwenyezi-Mungu wa majeshi, kuwa mtakatifu; utaniogopa na kunicha mimi peke yangu.

Isaya 8