Isaya 8:4-10 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Maana kabla mtoto huyu hajafikia umri wa kuweza kutamka: ‘Baba’ au ‘Mama,’ utajiri wa Damasko na nyara walizoteka huko Samaria zitapelekwa kwa mfalme wa Ashuru.”

5. Mwenyezi-Mungu aliongea nami tena, akaniambia,

6. “Kwa kuwa watu hawa wameyakataa maji ya Shiloa yatiririkayo polepole, wakafa moyo mbele ya mfalme Resini na mfalme Peka mwana wa Remalia,

7. basi, mimi Bwana nitawaletea mafuriko makuu ya maji ya mto Eufrate yaani mfalme wa Ashuru na nguvu zake zote; yatafurika na kupita kingo zake.

8. Utaingia nchini Yuda kwa nguvu na kufurika na kupanda mpaka shingoni; utaenea juu ya nchi yako yote, ee Emanueli!”

9. Unganeni enyi watu wa mataifa nanyi mtafedheheshwa!Sikilizeni enyi nchi za mbali duniani!Jiwekeni tayari na kufedheheshwa;naam, kaeni tayari na kufedheheshwa.

10. Shaurianeni pamoja lakini itakuwa bure;fanyeni mipango lakini haitafaulu,maana Mungu yu pamoja nasi.

Isaya 8