Isaya 56:10-12 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Maana viongozi wao wote ni vipofu;wote hawana akili yoyote.Wote ni kama mbwa bubu wasiobweka,hulala tu na kuota ndoto,hupenda sana kusinzia!

11. Hao ni kama mbwa wenye uchu sana,wala hawawezi kamwe kutoshelezwa.Wachungaji hao hawana akili yoyote;kila mmoja hutafuta faida yake mwenyewe.

12. Huambiana, “Njoni, twende kutafuta divai;njoni tunywe tushibe pombe!Kesho itakuwa kama leo,tena itakuwa sikukuu kubwa zaidi.”

Isaya 56