Isaya 38:15-20 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Lakini niseme nini:Yeye mwenyewe aliniambia,naye mwenyewe ametenda hayo.Usingizi wangu wote umenitorokakwa sababu ya uchungu moyoni mwangu.

16. “Ee Bwana, Sisi twaishi kutokana na yote uliyotenda,kwa hayo yote mimi binafsi pia ninaishi.Nirudishie afya, uniwezeshe kuishi.

17. Nilipata mateso makali kwa faida yangu;lakini umeyaokoa maisha yangukutoka shimo la uharibifu,maana umezitupa dhambi zangu nyuma yako.

18. Huko kuzimu mtu hawezi kukushukuru wewe;waliokufa hawawezi kukushukuru wewe.Wala washukao huko shimonihawawezi tena kutumainia uaminifu wako.

19. Walio hai ndio wanaokushukuru,kama na mimi ninavyofanya leo.Kina baba huwajulisha watoto wao uaminifu wako.

20. “Mwenyezi-Mungu ataniokoa.Nasi tutamsifu kwa nyimbo za vinubisiku zote za maisha yetu,nyumbani kwake Mwenyezi-Mungu.”

Isaya 38