Isaya 38:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Wakati huo, mfalme Hezekia aliugua sana karibu kufa. Ndipo nabii Isaya mwana wa Amozi, akamwendea, akamwambia, “Hivi ndivyo anavyosema Mwenyezi-Mungu: Panga mambo yako sawasawa katika nyumba yako kwa kuwa utakufa, hutapona.”

2. Hezekia akageukia upande wa ukuta na kumwomba Mwenyezi-Mungu,

3. akisema, “Ee Mwenyezi-Mungu, nakusihi ukumbuke jinsi nilivyokutumikia kwa uaminifu na kwa moyo wangu wote, na kutenda yaliyo sawa mbele yako.” Hezekia akalia kwa uchungu sana.

4. Kisha neno la Mwenyezi-Mungu lilimjia Isaya:

Isaya 38