Isaya 21:5-8 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Chakula kimetayarishwa,shuka zimetandikwa,sasa watu wanakula na kunywa.Ghafla, sauti inasikika:“Inukeni enyi watawala!Wekeni silaha tayari!”

6. Maana Bwana aliniambia,“Nenda ukaweke mlinzi;mwambie atangaze atakachoona.

7. Akiona kikosi, wapandafarasi wawiliwawili,wapandangamia na wapandapunda,na awe macho;naam, akae macho!”

8. Kisha huyo mlinzi akapaza sauti:“Bwana, nimesimama juu ya mnara wa ulinzi mchana kutwa,nimeshika zamu usiku kucha!”

Isaya 21