27. Mji Siyoni utakombolewa kwa haki,uadilifu utawaokoa watakaotubu humo.
28. Lakini waasi na wenye dhambiwote wataangamizwa pamoja;wanaomwacha Mwenyezi-Mungu watateketezwa.
29. Mtaionea aibu hiyo mialoni mliyoipenda sana;mtafadhaika kwa sababu ya bustani mlizofurahia.
30. Mtakuwa kama mwaloni unaonyauka majani;kama shamba lisilo na maji.
31. Wenye nguvu watakuwa kama majani makavu,matendo yao yatakuwa kama cheche za moto.Watateketea pamoja na matendo yao,wala hapatakuwa na mtu wa kuwaokoa.