Isaya 1:27-30 Biblia Habari Njema (BHN)

27. Mji Siyoni utakombolewa kwa haki,uadilifu utawaokoa watakaotubu humo.

28. Lakini waasi na wenye dhambiwote wataangamizwa pamoja;wanaomwacha Mwenyezi-Mungu watateketezwa.

29. Mtaionea aibu hiyo mialoni mliyoipenda sana;mtafadhaika kwa sababu ya bustani mlizofurahia.

30. Mtakuwa kama mwaloni unaonyauka majani;kama shamba lisilo na maji.

Isaya 1