1. Msikilizeni Mwenyezi-Mungu,enyi Waisraeli.Mwenyezi-Mungu anawashutumu wakazi wa nchi hii.“Hamna tena uaminifu wala wema nchini;hamna anayemjua Mungu katika nchi hii.
2. Kuapa, uongo, mauaji, wizi na uzinzi huzuka humo.Umwagaji damu hufuatana mfululizo.