1. Watu wa Efraimu wananirundikia uongo,na Waisraeli udanganyifu.Watu wa Yuda, wananiasi mimi Mungu Mtakatifu.
2. “Watu wa Efraimu wanachunga upepokutwa nzima wanafukuza upepo wa mashariki.Wanazidisha uongo na ukatili,wanafanya mkataba na Ashuruna kupeleka mafuta Misri.”
3. Mwenyezi-Mungu ana mashtaka dhidi ya Yuda;atawaadhibu wazawa wa Yakobo kadiri ya makosa yao,na kuwalipa kadiri ya matendo yao.
4. Yakobo akiwa bado tumboni mwa mama yake,alimshika kisigino kaka yake.Na alipokuwa mtu mzimaalishindana na Mungu.
5. Alipambana na malaika, akamshinda;alilia machozi na kuomba ahurumiwe.Huko Betheli, alikutana na Mungu,huko Mungu aliongea naye.