Hesabu 9:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kisha mnamo mwezi wa kwanza wa mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka Misri, Mwenyezi-Mungu aliongea na Mose katika jangwa la Sinai. Alimwambia:

2. “Waisraeli sharti waiadhimishe sikukuu ya Pasaka wakati uliopangwa.

3. Hii itakuwa siku ya kumi na nne ya mwezi huu; wakati wa jioni watafanya hivyo kufuatana na masharti na maagizo yake yote.”

4. Kwa hiyo, Mose akawaambia watu kwamba wanapaswa kuiadhimisha sikukuu ya Pasaka.

Hesabu 9