5. “Pokea matoleo haya ili yatumiwe katika huduma itakayofanywa kwa ajili ya hema la mkutano, uwape Walawi, kila mmoja kwa kadiri ya kazi yake.”
6. Basi, Mose akachukua magari na mafahali akawapa Walawi.
7. Wagershoni wakapewa magari mawili na mafahali wanne, kwa kadiri ya huduma yao,
8. na Wamerari wakapewa magari manne na mafahali wanane, kuwasaidia katika kazi zao zote chini ya uongozi wa Ithamari mwana wa kuhani Aroni.