Hesabu 22:19-21 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Lakini tafadhalini laleni hapa usiku huu kama wale wenzenu, nami nipate kujua atakachoniambia Mwenyezi-Mungu tena.”

20. Basi, Mungu akamjia Balaamu usiku huo, akamwambia, “Kama watu hawa wamekuja kukuita, nenda pamoja nao, lakini fanya tu kile nitakachokuambia.”

21. Balaamu akaamka asubuhi, akatandika punda wake, akaenda pamoja na hao maofisa.

Hesabu 22