Hesabu 2:4-10 Biblia Habari Njema (BHN)

4. kikosi chake kulingana na hesabu ni wanaume 74600.

5. Wale watakaofuata kupiga kambi baada ya watu wa Yuda watakuwa kabila la Isakari, kiongozi wao akiwa Nethaneli mwana wa Suari,

6. kikosi chake kulingana na hesabu ni wanaume 54,400.

7. Kisha kabila la Zebuluni, kiongozi wao akiwa Eliabu mwana wa Heloni,

8. kikosi chake kulingana na hesabu ni wanaume 57,400.

9. Jumla yote ya watu watakaokuwa katika kambi ya Yuda kulingana na makundi yao ni watu 186,400. Hao ndio watakaotangulia kusafiri.

10. “Kwa upande wa kusini, wale walio chini ya bendera ya kundi la Reubeni kulingana na makundi yao, kiongozi wao akiwa Elisuri mwana wa Shedeuri,

Hesabu 2