Hesabu 2:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mwenyezi-Mungu aliwapa Mose na Aroni, maagizo yafuatayo:

2. “Waisraeli watapiga kambi zao, kila mmoja akikaa mahali penye bendera yake, penye alama za ukoo wake. Watapiga kambi zao kulizunguka hema la mkutano.

3. “Wale watakaopiga kambi upande wa mashariki kuelekea mawio ya jua watakuwa kikundi cha watu walio chini ya bendera ya Yuda na kiongozi wao atakuwa Nashoni mwana wa Aminadabu,

4. kikosi chake kulingana na hesabu ni wanaume 74600.

5. Wale watakaofuata kupiga kambi baada ya watu wa Yuda watakuwa kabila la Isakari, kiongozi wao akiwa Nethaneli mwana wa Suari,

Hesabu 2