Hesabu 12:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kisha Miriamu na Aroni walianza kumsema vibaya Mose kwa sababu ya mwanamke Mkushi aliyekuwa amemwoa.

2. Wakasema, “Hivi kwani Mwenyezi-Mungu amezungumza kwa kumwagiza Mose peke yake? Je, hajazungumza nasi pia?” Mwenyezi-Mungu aliyasikia maneno hayo.

3. (Mose alikuwa mtu mnyenyekevu kuliko watu wengine wote waliokuwa duniani.)

Hesabu 12