Hesabu 1:48-52 Biblia Habari Njema (BHN)

48. kwa sababu Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose,

49. “Usihesabu kabila la Lawi wala usiwafanyie sensa kati ya watu wa Israeli;

50. bali utawateua wawe waangalizi wa hema la ushuhuda, vyombo vyake vyote na kila kitu kilichomo ndani yake; watakuwa wakilibeba pamoja na vyombo vyake vyote. Watahudumu humo ndani na kupiga kambi yao kwa kulizunguka.

51. Tena wakati wa hema kungolewa Walawi ndio watakaolingoa na wakati wa hema kusimikwa Walawi ndio watakaolisimamisha.

52. Waisraeli wengine wote watapiga kambi zao makundimakundi, kila mtu katika kundi lake na chini ya bendera yake.

Hesabu 1