3. Lakini Mwenyezi-Mungu ameniambia mimi nabii Hagai,
4. “Je, ni sawa kwenu kukaa katika majumba yenu ya fahari hali hekalu langu ni magofu matupu?”
5. Sasa, asema hivi Mwenyezi-Mungu: “Fikirini kama mnafanya sawa!
6. Nyinyi mmepanda mbegu kwa wingi, lakini mmevuna kidogo; mnakula, lakini hamshibi; mnakunywa divai, lakini hamtosheki; mnavaa nguo, lakini bado mnasikia baridi; mfanyakazi mshahara wake huwa kama umetumbukizwa katika mfuko uliotoboka.”
7. Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi: “Fikirini kama mnafanya sawa!