15. Nitamwaga ghadhabu yangu juu ya Pelusiumu,ile ngome inayotegemewa na Misri;na kuangamiza makundi ya Thebesi.
16. Nitaiwasha moto nchi ya Misri.Pelusiumu utashikwa na dhiki kubwa,ukuta wa Thebesi utabomolewa,nao Memfisi utakabiliwa na adui mchana wazi.
17. Vijana wanaume wa Oni na Pi-besethi watauawa kwa upanga,na wakazi wengine watachukuliwa uhamishoni.
18. Huko Tahpanesi mchana utakuwa gizawakati nitavunja mamlaka ya Misrina kiburi chake kikuu kukomeshwa.Wingu litaifunika nchi ya Misrina watu wake watachukuliwa mateka.
19. Ndivyo nitakavyoiadhibu Misri.Na watu watatambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu.”
20. Siku ya saba ya mwezi wa kwanza, mwaka wa kumi na moja tangu uhamisho wetu, neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia:
21. “Wewe mtu! Nimeuvunja mkono wa Farao mfalme wa Misri, nao haukufungwa ili uweze kupona na kuweza kushika upanga.