Ezekieli 29:1-9 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kumi, mwaka wa kumi tangu uhamisho wetu, neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia:

2. “Wewe mtu! Mgeukie Farao mfalme wa Misri, utoe unabii juu yake na nchi yote ya Misri.

3. Mwambie kuwa mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:Mimi nitapambana na wewe mfalme wa Misri,wewe mamba ulalaye mtoni Nili!Wewe unafikiri kwamba Nili ni wako,kwamba wewe ndiwe uliyeufanya!

4. Basi, nitakutia ndoana tayani mwako,na kufanya samaki wakwame magambani mwako.Nitakuvua kutoka huko mtoni.

5. Nitakutupa jangwani,wewe na samaki hao wote.Mwili wako utaanguka mbugani;wala hakuna atakayekuokota akuzike.Nimeutoa mwili wakouwe chakula cha wanyama wakali na ndege.

6. Hapo ndipo wakazi wote wa Misri watatambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu.“Waisraeli walikutegemea wewe ee Misri, lakini umekuwa dhaifu kama utete.

7. Walipokushika kwa mkono, ulivunjika na kutegua mabega yao. Walipokuegemea ulivunjika na kutetemesha viungo vyao.

8. Kwa hiyo, mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Nitazusha upanga dhidi yako na kuwaua watu na wanyama wako wote.

9. Kwa sababu umesema kuwa mto Nili ni wako, kwamba ndiwe uliyeufanya, basi, nchi yako, Misri, itakuwa tupu na jangwa. Ndipo watu watatambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu.

Ezekieli 29