Ezekieli 19:5-7 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Mama yake alipoona kuwa amechoka kungoja,matumaini ya kumpata yamekwisha,alimchukua mtoto wake mwingine,akamfanya simba kijana hodari.

6. Huyo alipokuwa amekua,akaanza kuzurura na simba wengine.Naye pia akajifunza kuwinda,akawa simba mla watu.

7. Aliziandama ngome za watuna kuiharibu miji yao.Nchi ikatishika pamoja na wakazi wake,kwa sauti ya kunguruma kwake.

Ezekieli 19