1. Neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia:
2. “Kwa nini mnarudiarudia methali hii katika nchi ya Israeli:‘Akina baba wamekula zabibu mbichi,lakini meno ya watoto wao yakatiwa ganzi!’
3. Lakini, kama niishivyo mimi Bwana Mwenyezi-Mungu, nasema kwamba methali hii haitatumika tena katika Israeli.
4. Jueni kwamba uhai wote ule ni wangu, uhai wa mzazi na uhai wa mtoto. Yeyote anayetenda dhambi, ndiye atakayekufa.