2 Wafalme 22:9-11 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Katibu Shafani, alimwendea mfalme na kutoa habari, akisema, “Watumishi wako wametoa fedha zilizopatikana katika nyumba halafu wamezikabidhi kwa mafundi wanaosimamia marekebisho ya nyumba ya Mwenyezi-Mungu.”

10. Kisha katibu Shafani, akamwambia mfalme, “Kuhani Hilkia amenipa kitabu.” Naye Shafani akakisoma mbele ya mfalme.

11. Mfalme aliposikia maneno ya Kitabu cha Sheria, alirarua mavazi yake.

2 Wafalme 22