2 Wafalme 19:21-25 Biblia Habari Njema (BHN)

21. Hili ndilo neno la Mwenyezi-Mungu alilosema kumhusu Senakeribu:Anakudharau, anakubeza binti Siyoni,anatikisa kichwa chake nyuma yako binti Yerusalemu.

22. Je, uliyekuwa unamkashifu na kumdhihaki ni nani?Nani umemwinulia sautina kumkodolea macho kwa kiburi?Juu ya Mtakatifu wa Israeli!”

23. Kwa kuwatuma wajumbe wako umemkashifu Bwana,wewe umesema, “Kwa magari yangu mengi ya vita,nimekwea vilele vya milimampaka kilele cha Lebanoni.Nimekata mierezi yake mirefu,na misonobari mizurimizuri;nimeingia mpaka ndani yakena ndani ya misitu yake mikubwa.

24. Nimechimba visimana kunywa maji mageninilikausha mito yote ya Misrikwa nyayo za miguu yangu.

25. ‘Je, hujasikia,kwamba nilipanga jambo hili tangu awali?Ninachotekeleza sasa nilikipanga zamani.’Nilikuweka uijenge miji yenye ngomekwa rundo la magofu.

2 Wafalme 19