2 Wafalme 11:19-21 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Aliwachukua makapteni, Wakari na wakazi wote; nao wakamsindikiza mfalme kutoka nyumba ya Mwenyezi-Mungu wakapitia katika lango la walinzi mpaka ikulu. Naye akakikalia kiti cha enzi.

20. Kwa hiyo, wakazi wote walijawa furaha; na mji wote ulikuwa mtulivu, baada ya Athalia kuuawa kwa upanga katika ikulu.

21. Yoashi alianza kutawala Yuda akiwa na umri wa miaka saba.

2 Wafalme 11