2 Timotheo 2:11-14 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Usemi huu ni wa kweli:“Ikiwa tulikufa pamoja naye,tutaishi pia pamoja naye.

12. Tukiendelea kuvumilia,tutatawala pia pamoja naye.Tukimkana,naye pia atatukana.

13. Tukikosa kuwa waaminifu,yeye hubaki mwaminifu daima,maana yeye hawezi kujikana mwenyewe.”

14. Basi, wakumbushe watu wako mambo haya na kuwaonya mbele ya Mungu waache ubishi juu ya maneno. Ubishi huo haufai, ila huleta tu uharibifu mkuu kwa wale wanaousikia.

2 Timotheo 2