43. Niliwatwanga na kuwaponda kama mavumbi ya nchi,nikawaponda na kuwakanyaga kama matope barabarani.
44. “Wewe uliniokoa na mashambulizi ya watu wangu,umenifanya mtawala wa mataifa.Watu nisiowajua walinitumikia.
45. Wageni walinijia wakinyenyekea,mara waliposikia habari zangu walinitii.
46. Wageni walikufa moyo;wakaja kutoka ngome zao wakitetemeka.