35. Hunifunza kupigana vita,mikono yangu iweze kuvuta upinde wa shaba.
36. Umenipa ngao yako ya kuniokoa;msaada wako umenifanya mkuu.
37. Umenirahisishia njia yangu;wala miguu yangu haikuteleza.
38. Niliwafuatia adui zangu na kuwaangamiza,sikurudi nyuma mpaka wameangamizwa.