1 Wakorintho 16:20-24 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Ndugu wote wanawasalimuni. Nanyi salimianeni kwa ishara ya mapendo ya Mungu.

21. Mimi Paulo nawasalimuni, nikiandika kwa mkono wangu mwenyewe.

22. Yeyote asiyempenda Bwana, na alaaniwe. MARANATHA – BWANA, NJOO!

23. Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.

24. Upendo wangu uwe kwenu katika kuungana na Kristo Yesu.

1 Wakorintho 16