1 Wakorintho 15:9-18 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Maana mimi ni mdogo kabisa miongoni mwa mitume, na wala sistahili kuitwa mtume, kwa sababu nililidhulumu kanisa la Mungu.

10. Lakini, kwa neema yake Mungu, nimekuwa kama nilivyo, na neema yake kwangu haikuwa bure. Mimi nimefanya kazi kuliko wote; si mimi hasa, ila ni neema ya Mungu ifanyayo kazi pamoja nami.

11. Lakini hata hivyo, iwe wao ndio wahubirio au mimi nihubiriye, haidhuru, hiki ndicho tunachohubiri, na hiki ndicho mnachoamini.

12. Sasa, maadamu inahubiriwa kwamba Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, baadhi yenu wanawezaje kusema kwamba hakuna ufufuo wa wafu?

13. Kama hakuna ufufuo wa wafu, basi, Kristo naye hakufufuka;

14. na kama Kristo hakufufuka, basi mahubiri yetu hayana maana na imani yenu haina maana.

15. Zaidi ya hayo sisi tungekuwa mashahidi wa uongo mbele ya Mungu, maana tulisema kwamba Mungu alimfufua Kristo kutoka kwa wafu na kumbe yeye hakumfufua – kama ni kweli kwamba wafu hawafufuliwi.

16. Maana, ikiwa ni kweli kwamba wafu hawafufuki, basi naye Kristo hakufufuka.

17. Na kama Kristo hakufufuliwa, basi, imani yenu ni ya bure; mngali bado katika dhambi zenu.

18. Zaidi ya hayo, wale wote waliokufa wakiwa wameungana na Kristo wamepotea kabisa.

1 Wakorintho 15