1 Wakorintho 15:11-14 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Lakini hata hivyo, iwe wao ndio wahubirio au mimi nihubiriye, haidhuru, hiki ndicho tunachohubiri, na hiki ndicho mnachoamini.

12. Sasa, maadamu inahubiriwa kwamba Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, baadhi yenu wanawezaje kusema kwamba hakuna ufufuo wa wafu?

13. Kama hakuna ufufuo wa wafu, basi, Kristo naye hakufufuka;

14. na kama Kristo hakufufuka, basi mahubiri yetu hayana maana na imani yenu haina maana.

1 Wakorintho 15