1 Wafalme 9:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mfalme Solomoni alipomaliza kujenga nyumba ya Mwenyezi-Mungu na ikulu na majengo mengine yote aliyokusudia kujenga,

2. Mwenyezi-Mungu alimtokea tena kama alivyomtokea kule Gibeoni.

3. Mwenyezi-Mungu alimwambia, “Nimesikia sala yako na ombi lako. Nimeitakasa nyumba hii ambayo umenijengea ili watu waliabudu jina langu hapa milele. Nitaichunga na kuipenda wakati wote.

1 Wafalme 9