1 Wafalme 17:4-7 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Huko, utapata maji ya kunywa katika kijito hicho tena nimewaamuru kunguru wakuletee chakula.”

5. Basi, Elia akatii agizo la Mwenyezi-Mungu, akaenda kukaa kwenye kijito cha Kerithi kilichoko mashariki ya mto Yordani.

6. Kunguru wakawa wanamletea mkate na nyama, asubuhi na jioni; akapata na maji ya kunywa katika kijito hicho.

7. Lakini, baada ya siku chache kijito kikakauka kwa sababu hapakunyesha mvua nchini.

1 Wafalme 17