1 Timotheo 2:11-15 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Wanawake wanapaswa kukaa kimya na kuwa wanyenyekevu wakati wa kujifunza.

12. Mimi simruhusu mwanamke amfundishe au amtawale mwanamume; anapaswa kukaa kimya.

13. Maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa.

14. Na wala si Adamu aliyedanganywa; bali mwanamke ndiye aliyedanganywa, akaivunja sheria ya Mungu.

15. Hata hivyo, mwanamke ataokolewa kwa kupata watoto, kama akidumu katika imani, upendo, utakatifu na unyofu.

1 Timotheo 2