11. Wanawake wanapaswa kukaa kimya na kuwa wanyenyekevu wakati wa kujifunza.
12. Mimi simruhusu mwanamke amfundishe au amtawale mwanamume; anapaswa kukaa kimya.
13. Maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa.
14. Na wala si Adamu aliyedanganywa; bali mwanamke ndiye aliyedanganywa, akaivunja sheria ya Mungu.
15. Hata hivyo, mwanamke ataokolewa kwa kupata watoto, kama akidumu katika imani, upendo, utakatifu na unyofu.