1 Mambo Ya Nyakati 23:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Daudi alipokuwa mzee wa miaka mingi, alimtawaza Solomoni mwanawe awe mfalme wa Israeli.

2. Mfalme Daudi aliwakusanya wakuu wote wa Israeli, makuhani na Walawi.

3. Walawi wote wanaume wenye umri wa miaka thelathini na zaidi, wakahesabiwa. Jumla yao ilikuwa 38,000.

4. Hao, Daudi aliwagawanya: 24,000 kati yao wawe wasimamizi wa kazi ya nyumbani kwa Mwenyezi-Mungu, 6,000 wawe maofisa na waamuzi,

1 Mambo Ya Nyakati 23