1 Mambo Ya Nyakati 16:8-12 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Mpeni shukrani Mwenyezi-Mungu,tangazeni ukuu wake,yajulisheni mataifa mambo aliyoyatenda!

9. Mshangilieni, mwimbieni Mungu sifa;simulieni matendo yake ya ajabu!

10. Jisifieni jina lake takatifu;wenye kumcha Mwenyezi-Mungu na wafurahi.

11. Mwendeeni Mwenyezi-Mungu mwenye nguvu;mwendeeni Mwenyezi-Mungu daima.

12. Kumbukeni matendo ya ajabu aliyotenda,maajabu yake na hukumu alizotoa,

1 Mambo Ya Nyakati 16