8. Mpeni shukrani Mwenyezi-Mungu,tangazeni ukuu wake,yajulisheni mataifa mambo aliyoyatenda!
9. Mshangilieni, mwimbieni Mungu sifa;simulieni matendo yake ya ajabu!
10. Jisifieni jina lake takatifu;wenye kumcha Mwenyezi-Mungu na wafurahi.
11. Mwendeeni Mwenyezi-Mungu mwenye nguvu;mwendeeni Mwenyezi-Mungu daima.
12. Kumbukeni matendo ya ajabu aliyotenda,maajabu yake na hukumu alizotoa,