1 Mambo Ya Nyakati 16:23-27 Biblia Habari Njema (BHN)

23. Mwimbieni Mwenyezi-Mungu, ulimwengu wote.Tangazeni kila siku matendo yake ya wokovu.

24. Yatangazieni mataifa utukufu wake,waambieni watu wote matendo yake ya ajabu.

25. Maana Mwenyezi-Mungu ni mkuu, anasifika sanaanastahili kuheshimiwa kuliko miungu yote.

26. Miungu yote ya mataifa mengine si kitu;lakini Mwenyezi-Mungu aliziumba mbingu.

27. Utukufu na fahari vyamzunguka,nguvu na furaha vyajaza hekalu lake.

1 Mambo Ya Nyakati 16