23. Mwimbieni Mwenyezi-Mungu, ulimwengu wote.Tangazeni kila siku matendo yake ya wokovu.
24. Yatangazieni mataifa utukufu wake,waambieni watu wote matendo yake ya ajabu.
25. Maana Mwenyezi-Mungu ni mkuu, anasifika sanaanastahili kuheshimiwa kuliko miungu yote.
26. Miungu yote ya mataifa mengine si kitu;lakini Mwenyezi-Mungu aliziumba mbingu.
27. Utukufu na fahari vyamzunguka,nguvu na furaha vyajaza hekalu lake.